SALON


NAMNA NZURI YA KUOSHA NYWELE ZAKO

KUNA kitu muhimu kuhusu uoshaji wa nywele, nywele zako ambazo unataka zikae unavyotaka kulingana na kichwa chako ili uwe na uvuto wa haiba yake katika mambo yote yanayokuzunguka.
katika mazingira ya kawaida uoshaji nywele ni kitu cha kawaida na hivyo mara nyingi hatufikirii sana suala la kuosha nywele, si la kawaida tu mwenzangu? Lakini uoshaji nywele wa uhakika wenye makini kwa kutumia shampuu kunaweza kuleta mabadiliko makubwa katika muonekano na umetaji wa nywele zako na hata makuzi yake.
Ndio kusema uoshaji wa kutumia shampuu unaweza kabisa kukupa kile ambacho huwezi kukipata katika hali ya kawaida , muondoko wa ukaaji wa nywele baada ya kuosha.
Lakini kama hutajali tulijadili hili suala la uoshaji nywele ambalo ni la kawaida tu.Naama, la kawaida lakini lenye maana kubwa kwa watu wanaojijali.
Mimi nadhani haitaumkiza kama nikisema kwa ufupi fupi kuhusu hizi shampuu za kuonshea nywele, hizi shampuu ambazo unazipata dukani, kwenye dula la urembo.
Kwanza ni lazima utambue kwamba si kila shampuu inafaa katika kusuklia nyweleza ko (uoshaji) kwani nyingine huleta mushkeri hasa kama unaumwa eczema, hali ya kuchoma choma, uwasho wa nywele, mba au aina ya grisi katika ngozi ya nywele zako wakati wa kuzitengeneza.
Nataka kukuambia kwamba bidhaa zinazotokana na uasili husaidia sana kutengeneza utamu wa nywele kama kweli unaujua na mara zote hufanyakazi bora kwa aina zote za vichwa hata kama zina matatizo niliyotaja hapo juu.
Na pia huleta aina ya burudiko.
Mara zote tunapoosha nywele zetu huwa tunaharibu lakini kama utakuwa mwangalifu kwa kutumia shampuu zenye viambata vya asili (organiki-natural botanical)utakuwa na nafasi kubwa ya kuwa na nywele tamu na wewe kuondokana na adha za uchafu wa nywele unaotia 'wazimu'.
Kama utakuwa huna shampuu ile ya dukani ambayo ina aviambata vya asili nashauri utumie yai. yai ni kifaa kizuri kabisa cha kusafishia.tenganisha kiini cha yai kutoka katika uite mweupe. konga tofauti kisha changanya na taratibu zitumie kuzichanganya katika nywele ne kusukasuka. Acha kwa dakika tatu na kisha safisha kwa maji ya uvuguvugu si ya moto kwani ukitia maji ya moto yao litajikusanya maeneo fulani fulani kichwani halafu itakuwa shida.
Njia tano za kuosha nywele zako:
1.Inama katika beseni. Hii inasaidia kutoa nafasi ya ukaaji mzuri wa kuanza kusafisha nywele bila kuumiza shingo yako na pia kusaidia kuweka damu katika mzunguko unaotakiwa.
2.Tumia kikombe kimoja cha shampuu. Ikiwa nyingi italeta matatizo kidogo na kidogo pia haitatoa kitu kinachostahili. pakaza kwa kusukasuka kila mahali kichwani mwako kwa kuanzia mbele kwenda nyuma na kisha pembeni. Kwa nywele za grisi(mafuta) changanya shampuu na maji kidogo.
3. Tumia ncha ya vidole vyako kufika mwisho wa nywele na kuzimasaji vyema kuhakikisha kwamba shampuu inaingia katika ngozi ya kichwa. Safisha kwa raha kwani inatakiwa ujisikie raha kubwa wakati wa shughuli hii ya kusafisha nywele.
4.Hakikisha kwamba umesafisha sawasawa kichwa chako kisha unaondoa shampuu kwa maji..Kitu cha maana ni kuwa usafishaji lazima ufanyike kwa uangalifu mkubwa kwani baada ya kutia shampuu na kuipeleka kila mahali kuiondoa baada ya hapo ni kitu muhimu.Iondoe kwa maji na kisha kujihakikisha kwamba imeondoka, unastahili kukitia kichwa chako maji ya baridi kwa ajili ya kutoa busti zaidi.
5.Kausha nywele zako kwa taulo safi (kwepa kusugua nywele hizo kwa
taulo).Kifunike kichwa na taulo hilo ili linyonye maji taratibu na baada ya hapo unaweza kutia kitu kinachotakiwa ili kuweka nywele za safi

MAISHA , MAPENZI, UREMBO

Maisha yetu ya kila siku yana vitu vingi sana, vizuri kiasi kwamba unaweza furahi hadi ukajiuliza KWANINI NILICHELEWA kuanza????Na kuna vingine ni vibaya, kiasi kwamba unaweza kulia hadi ukajutia kwanini ulisema YES I DO.. njooni tuzunguze, tuongee, tushauriane,,tuone jinsi gani tunaweza kuboresha maisha haya wote tukayafurahia

HAYA, KWA WALE WALIOHITAJI VITU NINAVYOTUMIA KATIKA KUJAZA,KUKUZA NA KUPENDEZESHA NYWELE ZANGU

Kwa leo ninawaambia ni nini na tumia, ila nitaandaa picha za hivyo vitu pia ili niwatumie wiki ijayo,
Dawa ninayotumia ni Olive Oil,  zipo za aina tatu, na zote ni bidhaa za olive, na ambayo huwa naitumia sana ni ile yenye picha ya mtoto kwenye box, ambayo ndani yake ina kikopo kidogo cha steaming



Natumia Avocado shampoo, ni nzuri sana, lakini hata kama utaikosa kwenye haya masalon yetu waweza tumia shampoo yeyote ile,  mradi nywele zioshwe na zitakate, na pia tutumie conditioner, baada ya kuosha na shampoo, conditioner inasaidia sana kulainisha nywele na kuzuia zisikatike wakati wa kuchana, ni muhimu sana kuwa nayo, kama kwenye masalon yetu hakuna, basi nunua kifumu au kopo lako then unakuwa ukienda salon unamimina kidogo unakwenda nayo,
Huwa natumia mayonise steaming,  hii pia ziko za aina mbili, kuna le kubwa kabisa ambayo ni white cream, na kuna kubwa kias ambayo ni dark cream, I mean cream iliyokolesa sanaaaaa,
Sasa hii iliyo koleza sana ndio huwa natumia, na ninaitumia kila wiki, yani kila juma pili lazima nifanye steaming
                                      
Baada ya kuosha nywele zangu toka kwenye steamer kabla ya kupaka pinki lotion na kuanza kuseti huwa napaka kwenye ngozi ile steaming iliyopo ndani ya dawa,  naipaka kwenye ngozi tu! Kisha inachanganywa, halafu ndio unapaka pinki lotion kiasi tu(hii haioshwi, unasetia

Baada ya nywele kukakuka huwa natumia Blue magic chafu, wenyewe wauzaji wanaita blue magic ya chenga, inapakwa kwenye ngozi, na juu, kama ukikosa tumia hata Venus, but  blue magic ni nzuri zaidi naona inajaza sana nywele, inalainisha, na kuzifanya zikae wiki nzima zikishine, coz mimi huwa nikipaka jumapili sipaki tena hadi jumapil ingine na nywele huendelea kulegea na kubaki katika mvuto wake

HIVYO NDIO VITU NINAVYOTUMIA KICHWANI KWANGU

ADDITION

1.     Usisubiri harusi au sikukuu ndio uende salon, jitahidi kila wiki, au kama utashindwa basi atleast mara mbili au tatu kwa mwezi

2.     Kata ncha za nywele zako kidogo kila baada ya miezi miwili unapotoka kuretouch

3.     Usisuke nywele siku chache baada ya kuretouch, utazikata,  acha ziotee kwanza ndio usuke,

4.     Usifumue nywele kama unagombana, fumua taratiibu, kama umesikuka kimasai basi ikibidi chambua nywele moja moja kwa kutumia sindano,

5.     Usipende sana kutumia loterbody au jerry, hii inakata sana nywele labda kuwe na sababu maalum ya kufanya hivyo, lakini, mh! Sishauri sana
6.     Kwa wale wapenda rangirangi kama mimi, unapoweka breach, usifikishe kwenye ngozi, (shina la nywele) breach inapakwa kwa juu tu!

7.     Pia wale wa kutong, ni nzuri sana kutong kwa kutumia rolas au mabomba ya mipapai au mirija ya juice, lakini kutong kwa kutumia mashine, sio kuzuri sna  sababu mashine inaunguza nywele, 

8.     Usiwejiweke dawa mwenyewe kama sio mtaalamu au usimpe mtu asielewa namna ya kuweka dawa , atafanya zikatike, that’s  whay unashauriwa kwenda salon,


Kuna uwekaji wa aina mbili,
a)     Kwa wenye nywele nyingi na kavu hadi juu, unaporetouch anza chini, then katika kuchanganya apake hadi juu ili kulainisha zile za juu, 


b)    Kwa wale wenye nywele chache, na laini, unaporetouch usifikishe dawa juu utazimaliza, weka dawa chini tu! Kule kuliko otea, na kama ni chache halafu kavu, basi rambisha kidogo kwa juu dakika kumi au 15 kabla ya kuosha,
c)     Jitahidi unaporetouch usiwe na Mba nyingi kichwani, maana zinasababisha kuungua sana na kung’oka nywele kutokana na majeraha,

PAMOJA NA VYOTE HIVYO, NYWELE ZINAHITAJI USAFI SANA, ILI ZIPATE NAFASI YA KUKUA VIZURI, HATA KAMA UMESUKA UNAWEZA KWENDA SALON UKAOSHA NA KUKAUSHA, HIZO NYWELE ULIZOSUKA

4 comments:

  1. Nimefurahi sana kwa maelezo yako,unaweza niambia nywele ngumu zinahitaji steaming ya aina gani?

    ReplyDelete
  2. Ahsante kwa ushauriwako sasa nimeelewa sana juu ya utunzaji wa nywele

    ReplyDelete
  3. Jaman mm siweka dawa ila hapo kwenye blue magic ni fire natumia hay mafuta mm bas nywele zangu nikizifumua zimejaa na ni ndefu sio poa

    ReplyDelete
  4. Conditioner unatumia ya Aina gani

    ReplyDelete